• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Saturday, December 10, 2016

Angalia hapa na Ujifunze Umaridadi mwingine kwa Uzio wa Nyumba yako

Kadiri teknolojiainavyokuwa ndivyo na ubunifu wa mapambo ya nyumba huongezeka. Leo nakusogezeapicha hizi mbili zikionesha urembo mzuri na geti lililopambwa vizuri kuanzia muundo wake na finishin zilizvyofanywa.

Picha ya chini ni rough plaster kwenye ukuta wa tofali kama inavyoonekana. Ukihitaji ufundi wa namna hii ususite kuwasiliana nasi kwa nambari 0757718080 na kuona namna ya kusaidiana kupata kilicho bora! Karibu sana




Saturday, November 26, 2016

UKO DAR!? UNAHITAJI MAGETI YA KISASA YA KUSLIDE? WAONE UZ METAL WORKS

MAGETI YA KISASA YA KUSLIDE @ UZ METAL WORKS

Uwapo Dar es Salaam mjini usiwaze wapi utapata mageti mazuri ya kuslide.gharama zinaanzia sh 1.6m na kuendelea .Tuko Mwenge ITV na Goba Tatedo Dsm. Simu 0786808707

Saturday, November 19, 2016

Nini suluhu ya ujenzi holela katika miji yetu?




Ukitembelea maeneo mengi  ya miji  yanayokua utakuta nyumba za makazi zimejengwa kwa kusongana sana kiasi cha kushindwa kuruhusu huduma za dharura kama gari la wagonjwa ama la kuzimia moto kutoweza kufika kila mahali.

Hatari ya moto pia huwa kubwa zaidi kuambikiza nyumba nyingine zilizo jirani  kutokana na zilivyosongana.

Kama picha  inavyoonesha ndivyo ambavyo  maeneo mengi  ya makazi yamejengeka. Hakuna uhuru  wa kupita  na hata utambuzi wa nyumba unakuwa mgumu.

Kadiri miji  inavyokuwa na kuhitaji maboresho ndivyo ambavyo  adha  ya kusongamana huku inavyoonekana. Kwa mfano, upanuzi na uboreshaji wa barabara kwa viwango vya lami unapata changamoto ya kukosa eneo la kutosha kujenga barabara nzuri na huduma za waenda kwa miguu.

Harakaharaka, haya yanatokana na maeneo hayo kutopimwa na watu pengine  kutoka na na kipato duni wanaamua kujijengea kadiri anavyopata kijieneo.

Unadhani kuna suluhisho zaidi tofauti na maeneo kuwa yamepimwa na wananchi kutakiwa kujenga kwa kufuata mpango  wa mji!?

Wednesday, November 16, 2016

Je, Unaweza Kutofautisha Kati ya Lenta na Bimu (lintel & beam) kwenye nyumba!? Soma hapa

Watu wengi huwa wanapata ugumu wa kutofautisha kati ya "beam"au bimu na "lintel" au lenta kwenye ujenzi wa nyumba. Wapo baadhi ya mafundi pia wanajichanganya katika hili. Baada ya kusoma hapa na kuangalia picha hizi natumaini utakuwa umeweza kujua tofauti halisi. 

Kabla ya kuangalia tofauti zake, bimu ama leta zinaweza kujegwa kwenye jengo kwa kutumia 'material' za  aina tofauti. Hebu kwanza tuangalie kila kimojani kitu gani ndipo tuweze kuona tofauti baina yao..

Lintel ama lenta ni nini!? 

Lenta ni memba ya jengo ambayo huwekwa juu ya uwazi wa ama mlango au dirisha na kadhalika kama picha hizi zinavyoonesha. Unene wa lenta mara nyini huwa sawa na unene wa ukuta husika, na kina chake (depth) kinaweza kuwa mm 100, 150 au zaidi kidogo.

Lenta zipo za aina nyingi kama nilivyoeleza awali, kama vile 
(a) Lenta ya zege na nondo
(b) Lenta ya matofali ya ya kawaida au ya kuchoma
(c) Lenta ya mawe
(d) Lenta ya mbao, ama
(e) Lenta ya chuma

Bimu (beam) ni nini kwenye nyumba?
Bimu ni memba ya jengo inayobeba uzito unaosambaa kufuata mzunguko wajengo, na hutofautishwa kutegemeana na vitu kama
(a) Upana wa ndani kwa ndani kutoka kwenye egemeo moja na jingine la ukuta
(b) kiunganishio cha kubeba kenchi au sakafu (floor) zinazoning'inia
(c) Kama Girders, ambapo zinafanya kazi kama jukwaa la kubebea sakafu (vibeba uzito)
(d) Spandrels. Hizi ni bimu ambazo ziko kwanje usawa wa floor zikiwa mhsusikubeba sehemu ya uzito/mzigo wa sakafu kupeleka ukuta wanje. 
(e) Dead load beams, hizi huwa mahsusi kubeba mzigo wote wa jengo lenyewe na kuupeleka kwenye nguzo za jengo (columns kwa ajili ya kuushusha ardhini
(f) Live load beama, ambazo hubeba uzito unaotokana na nguvu ya nje inayoshukia kwenye jengo

Yote kwa yote, kwa kawaida bimu ziko za aina zifuatazo
(a) Simply supported beam 
(b) Cantilever beam (iliyoshikiliwa upande mmoja)
(c) Rigidly fixed beam (iliyosikiliwa vizuri)
(d) Over hanging beam (inayoning'inia)

Kuhitimisha somo letu, kwa lugha rahisi zaidi, bimu inajitofautisha na lenta kwa maana kwamba yenyewe huwana kazi kubwa ya kubeba uzito kwenye jengo na wakati mwingine huzunguka jengo zima wakati lenta yenyewe huwekwa juu ya uwazi wa mlango ama dirisha kwaajili ya kufanya uwazi huo uwepo na kwajuu yake ukuta uendelee. Pichanini mbao zimetengenezwa kuwezesha kutengeneza bimu ya zege na nondo kuzunguka nyumba nzima. 












Tuesday, November 15, 2016

KUTANA NA MBUNIFU MAJENGO EDWARD KAYOMBO HAPA! ISHI KATIKA NDOTO YAKO

Leo nimekusogeza karibu na mtaalamu wa ubunifu wa majengo ya aina mbalimbali. Anafahamika kama Edward Kayombo na kama utakuwa umefurahia moja ya kazi zake unaweza mcheki kwa nambari 0762 965 587. Ikikosekana unaweza kuwasiliana nasi kwa 0757718080 tukakusaidia kupata ukitakacho! Karibu sana.
Baadhi ya kazi zake za ubunifu ni hizi hapa chini

















Thursday, November 3, 2016

Waziri Lukuvi - Asilimia 85 ya Ardhi nchini haijapimwa,Watu wengi wanaendelea kuishi katika makazi holela

Hayo ameyasema leo Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi wakati akifungua Mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi uliofanyika jijini Dar es Salaam, amesema kuwa wataalam wafanye kazi ya kupima ardhi ili kuweza kuondokana na makazi holela.

Amesema kuwa serikali inapoteza mapato kutokana na kuwa na sehemu kubwa ya ardhi kutopimwa.Lukuvi amesema wapimaji wa sekta binafsi wamekuwa wakifanya vizuri kuliko wale ambao wameajiliwa na serikali.

Amesema lazima kuondokana na mfumo wa hati kwenye karatasi na kuingia katika mfumo wa kieletroniki katika kusaidia wananchi kudhulumiwa ardhi kwa kushirikiana na watumishi wasio waaminifu.

Waziri Lukuvi amesema ni marufuku kwa wapimaji ardhi walioajiliwa na serikali kuwa kampuni za upimaji wa ardhi ili kuondokana na mgongano wa kimasilahi. Amesema katika miaka 10 ijayo kuwa kila mtu kuwa hati na kiwanja au shamba kiwe kimepimwa.Lukuvi amesema katika kuondoa migogoro ya wafugaji ni kuondokana na uchungaji wa mifugo.

Amesema kufika mwishoni mwa mwaka huu wawe wamepima ardhi viwanja 400.Nae Rais IST, Martins Chodata amesema kuwa watashirikiana na serikali katika masuala ya upimaji ardhi.Amesema wapo baadhi ya wapimaji ardhi hawana maadili na kusababisha kuwepo migogoro. 

Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akifungua mkutano mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi linalofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia leo Novemva 2-3, 2016.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akionyeshwa moja ya vifaa vinavyotumika katika upimaji wa Ardhi mapema leo katika Mkutano mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi unaofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akipewa maelezo jinsi mambo yalivyobadirika katika mfumo wa Kidigitali.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akiwa amebeba moja ya kifaa kinachotumika katika upimaji.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akionyeshwa kifaa cha kisasa kinachotumika katika upimaji.
Wapimaji wa Ardhi wakiwa katika mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi.
Wapimaji wa Ardhi wakiwa katika mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi.
Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akitoa cheti cha shukrani kwa makampuni yaliweza kusaidia kufanikisha mkutano Mkuu na Kongamano la Wapimaji Ardhi. Pembeni kushoto ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani, Bw. Justo Lyamuya.

Friday, October 21, 2016

TASWIRA: RAIS MAGUFULI ALIVYOWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI HOSTEL ZA WANAFUNZI UDSM


Leo October 21 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Mwezi Juni mwaka huu wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho.
Wakati Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi la mradi huo, tayari ujenzi umefikia asilimia 75 ambapo majengo 20 yaliyounganishwa kimuundo yamefikia ghorofa ya nne na ujenzi huo unaofanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Desemba, 2016.
Rais Magufuli ameahidi kuwa, kwa kuwa majengo hayo yanauwezo wa kubeba ghorofa sita, Serikali itafanya utaratibu wa kutumia moja ya likizo za wanafunzi kuongeza ghorofa nyingine mbili ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata nafasi.
1
Rais Magufuli akikata utepe kabla ya kuweka jiwe la msingi
1
5
Rais Magufuli na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandara

7
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania TBA Arch. Elius Mwakalinga akitoa ufafanuzi kwa Rais Magufuli kuhusu ujenzi wa Hosteli
7

PICHA ZOTE NA MAELEZO: MILLARDAYO.COM

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA: UTARATIBU WA UTOAJI VIBALI VYA UJENZI

Kibali cha ujenzi ni  kibali kinachotokewa na mamlaka za Miji  ama Majiji chini ya sheria ndogo za Udhibiti wa ujenzi Mjini. Kibali hiki kinatolewa ili kumruhusu Mwananchi afanye ujenzi au ukarabati wa jengo mahali fulani  katika eneo la mji  husika.

Katika makala  ya leo, nakupitisha kwenye tataribu za kufuata ili kupata kibali cha ujenzi kwa kuangalia tataribu na kanuni za utoaji vibali hivyo kwa Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Kabla ya hapo, kwanza tuangalie kwa pamoja umuhimu wa kupata kibali cha ujenzi.
1. Kutimiza matakwa ya sheria ndogo za Jiji
2. Kuwezesha kujenga majengo na nyumba kwa kuzingatia maelekezo ya mipango miji
3. Kudhibiti ujenzi holela na miji  isiyopangika

Kanuni za Utoaji wa Vibali vya Ujenzi na Hatua za Kufuata
Hatua hizi zinaanza baada ya kuwa umeshakamilisha michoro ya jengo lako
1. Kuwasilisha michoro iliyokamilika na kujaza fomu maalumu inayotolewa na Halmashauri, fomu ambayo inajumuisha maoni ya wataalamu wafuatao
a. Mkaguzi wa Majengo wa Jiji  (Building Inspector)
b. Afisa Ardhi wa Jiji (City Land Officer)
c. Mpima Ardhi wa Jiji (City Land Surveyor)
d. Afisa Mipango Miji  wa Jiji (City Town Planning Officer)
e. Afisa Afya wa Jiji (City Health and Sanitation Officer)

2. Ukishawasilisha michoro iliyokamilika pamoja na kujaza fomu niliyotaja hapo juu, fomu itaambatanishwa na michoro husika (architectural na structural drawings) na kupita  kwa wataalamu wote  niliotaja kwa ajili  ya uhakiki.

Wataalamu hao watapitia maombi yako na michoro na kujiridhisha yafuatayo.
a. Mkaguzi wa Majengo wa Jiji ataangalia kama michoro inakidhi haja ya kiufundi na masuala mengine ya kitaalamu
b. Afisa Ardhi wa Jiji ataangalia kuona kama umiliki wa eneo unalotaka kufanya ujenzi ni  halali na umiliki wake ni  sahihi
b. Mpima Ardhi wa Jiji atajiridhisha na mipaka halali ya eneo unalotaka kuendeleza
c. Afisa Mipango Miji  atajiridhisha kama ujenzi unaoombewa kibali ni  sahihi kwa mujibu wa michoro ya mipango  miji  kuendana na matumizi ya ardhi  ya eneo husika
d. Afisa Afya wa Jiji atajiridhisha kuona kama usafi kwa ujumla na mfumo wa maji taka umezingatiwa

3. Kama nyaraka za umiliki zimekidhi vigezo, zitawasilishwa kwenye Kamati ndogo ya Mipango Miji  na utoaji vibali 

4. Endapo muombaji utakuwa  umekamilisha hatua zote muhimu kwa wakati, kibali cha ujenzi kitapatikana ndani ya majuma mawili hadi  manne.

Kumbuka, michoro unayotakiwa kuwasilisha ni  ile ambayo imethibitishwa na wataalamu wabunifu wa michoro ya ujenzi ikiwa na mihuri halali, sambamba na kuwa na hati sahihi za umiliki wa eneo. Ukikamilisha haya zoezi linakuwa rahisi sana.

Makala ijayo tutaangalia ni  madhara na hatari gani inaweza kukukumba endapo utajenga au kukarabati jengo lako ndani ya Jiji la Arusha bila kibali toka Halmashauri ya Jiji.


Sunday, August 14, 2016

Mkutano Mkubwa Afrika wa Wataalamu wa Ujenzi Kufanyika Agosti 18&19 Dar es Saalam.. Jiandikishe Ushiriki!


.


Sunday, July 10, 2016

Madirisha ya Aluminium yenye pannel ndogo na muonekano mzuri

Dirisha la aluminiam kala ya kuondolewa "frame protectors"
Zoezi la kufitisha madirisha likiwa linaendelea

Tangu teknolojia ya matumizi ya bidhaa za aluminium na glasses yaingie nchini, kumekuwapo na muundo unaofanana wa madirisha ya nyumba yakiwa na sliding casement kubwa kidogo. Mara nyingi ni aidha vipande viwili au vitatu sambamba na ventlight kwa juu.

Leo nakusogezea ubunifu mwingine wa bidhaa hizi ambapo nakuunganisha na wataalamu kama picha  za kazi zao zinavyoonesha hapo juu.

Co:Purity Company
Style:box box
Price: per sq.m 130,000/=
Glass used : t.bronze

Mawasiliano: 0715 252162


Matumizi ya Chuma badala ya Mbao kupaua nyumba. Soma hapa!



Katika kiondokana na adha ya uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ili kupata mbao za kujengea, teknolojia mpya ya kupauwa nyumba kwa kutumia chuma chepesi imeingia sokoni!

Chuma hizi nyeepesi kabisa na imara, zinakuepusha na hofu ya mchwa na paa kushuka kwa kuharibika mapema. Uimara wake ni wa kiwango cha juu. Hakishiki kutu, ni chepesi, kinafungika kirahisi,  imara kwa  paa, na linahimili janga la moto. 

Kwa wanaohitaji chuma hiki wawasiliane na Mr. Quality East Africa Ltd kwa simu 0659781978

Endelea kutembelea blogu yako hii itakukutanisha na wataalamu mbalimbali na wabunifu wa bidhaa na mitindo ya ujenzi.