Header Ads

Header Ads

Huyu Ndiye Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi !? Soma hapa kufahamu kazi zao.

Mabweni ya wasichana kwenye Shule ya Sekondari Mubaba Wilayani Biharamulo yaliyojengwa kwa kutumia matofali ya kufungamana ikiwa ni sehemu ya usambazaji wa teknolojia hiyo. PICHA NA NHBRA
Tanzania kama zilivyo nchi nyingine zinazoendelea imekuwa ikikabiliwa na upungufu wa nyumba bora. Kwa miongo mingi Serikali zote kabla na baada ya uhuru zilitambua matatizo ya nyumba, umuhimu na uharaka wa kuyatatua.

Juhudi mbalimbali zimefanywa kushughulikia tatizo hilo. Ilifikiriwa kwamba ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili ni kuunda taasisi zitakazokuwa na wajibu wa kutoa mafunzo katika sekta ya nyumba ili kuboresha na kuongeza msingi wa ubora wa nyumba kutokana na tatizo kuendelea kuwapo. Serikali iliamua kuunda upya kituo cha Utafiti wa Ujenzi (BRU), kuwa Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA), yenye mamlaka ya kuendesha shughuli kibiashara.

Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi umejikita katika kufanya utafiti katika maeneo yafuatayo:- Mbinu za ujenzi, Vifaa vya ujenzi, Gharama za ujenzi na usanifu majengo na Uchumi na kijamii.

Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi ni Wakala ya Serikali iliyoanzishwa tarehe 1 septemba 2001. Wakala hii iko chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ofisi zake ziko Mwenge barabara ya Sam Nujoma Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, umbali wa mita 400 kutoka barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

KAZI ZA NHBRA
Kufanya utafiti kuhusu nyenzo za ujenzi na teknolojia ya ujenzi katika ngazi ya matumizi
Kushirikiana na Mamlaka za Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mashirika ya Kijamii, Wabia wa maendeleo na watu binafsi katika kuunda na kutoa mafunzo kwa /vikosi vya ujenzi wa nyumba na uzalishaj vyenzo katika ngazi ya wananchi.
Kuhamasisha kujenga uwezo (k.v kiufundi, kifedha na kiuongozi) wa watendaji wanaohusika na maswala ya nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Kuhakikisha kuwa mipango, sheria, kanuni za ujenzi, viwango na udhibiti vinalingana na uwezo, mahitaji, matakwa na matarajio ya sekta mbalimbali za wananchi
Kuhamasisha uzalishaji na matumizi ya vifaa vya ujenzi vya hapa nchini na vya gharama nafuu
Kuonyesha kwa vitendo matumizi ya vifaa vya ujenzi vya nchini
Kushauri serikali na wananchi mambo yanayohusu maswala ya maendeleo ya makazi

KWA MENGI ZAIDI KUHUSU WAKALA HUYU TEMBELEA TOVUTI YA NHBRA HAPA

No comments: