Header Ads

Header Ads

MWONGOZO WA KUCHAGUA RAMANI BORA YA NYUMBA

Ramani ya nyumba-Mali ya P.Joseph

Bila shaka kila mmoja wetu anatamani kumiliki nyumba yake,na bila shaka wale ambao wamekwisha jenga wana ndoto za kujenga tena ama kuwashauri ndugu na marafiki kujenga.

Ujenzi katika sehemu kubwa ya Tanzania haufuati taratibu na sheria za ujenzi wa makazi.Zipo sababu nyingi ambazo zinasababisha hili lakini kwa leo mjadala utajikita katika namna ya kuchagua ramani bora ya nyumba

Ramani ya nyumba ni dira ambayo ni kazi ya usanifu yenye kuleta picha ya uhalisia utakaofikiwa na kutarajiwa na mteja.Kazi hii hufanywa na msanifu majengo amnbaye kwa lugha ya kiingereza huitwa Architect.

Msanifu husikiliza kwa makini matarajio ya mteja na kuiweka picha ya matarajio katika mchoro (picha).Watu wengi hudhani kazi ya Architect ni kuchora tu ramani,na ndio maana wengi hudhani ni jambo rahisi.Ukweli ni kwamba kazi yake ni kusanifu mawazo ya mteja na kuyaweka kuwa halisi.Kwa maana hiyo,hii ni fani ambayo huitaji umakini na elimu ya kutosha ili kuhakikisha anasanifu jengo ambalo litafanya wanaoishi waishi wakiupata msawazo katika joto,hewa,mwanga na wawe na furaha na kupapenda wanapoishi.

Baada bya maelezo hayo sasa tujiulize je,ramani bora inazingatia mambo gani?Ijulikane kwamba nimejaribu kupitia vigezo vitakavyomfanya kila mtu aelewe

Kwa wale ambao wana mpango wa kujenga nyumba bora za kisasa,mambo
yafuatayo ni muhimu kuyazingatia unapochagua ramani bora kwa ajili ya
nyumba yako: 
Mchoro ukionesha uhusiano uliopo kati ya sehemu moja na nyingine katika eneo (site plan).Picha ni mali ya Nyumba BoraTz


1.Izingatie maono ya mteja (client)-client imaginationikiwa na maana,mteja anapaswa kupata kile anachokipenda na alichofikiri kichwani kwake eitha kwa kuona ama kwa kutarajia 

2.Iwe na uhusiano mzuri kati ya eneo na eneo (mfano sebule na dining,dining na
jiko, sebule na vyumba.

3. Izingatie matumizi bora ya ardhi kwani ardhini gharama ( iwe na mgawanyo bora kati ya eneo linalojengwa, eneo amanafasi ya kutembea (circulating space), eneo la kijana (green
zone)-ama eneo linalopandwa miti, maua na vingine vyenye kuleta uhai.Ni lazima iepuke uwepo wa sehemu zisizo na kazi (dead space)

4.Izingatie hewa na mwanga wa kutosha katika kila eneo linalotumika,nanyumba bora huzingatia hewa na mwanga wa asili na sio artificial air.(viyoyozi)

5.Izingatie uwepo wa sitiri (privacy) –ihakikishe kila mtumiajianakuwa na uhuru wa kutosha na kuepuka muingiliano

6. Izingatie kuliendeleza eneo, lisiwe mfu kwa maana ya kuliharibu ama kuondoa vitu
vya msingi ambavyo vinafanya ardhi iwe oevu/endelevu 

7. Iwe inazingatia kufikika na matumizi kwa watu wa umri wote na maumbile yote mfano wazee,walemavu. 

8. Uzingatie uzuri- iwe inavutia (appealing to eyes) na wakati Fulani mvuto wake uwe wa kipekee ama mfano mahali inapojengwapo, iwe kioo cha eneo,utamaduni na mazingira ya eneo.

9.Izingatie matumizi bora ya maji na nishati,ikihusianisha vema sehemu zinazohitaji matumizi ya maji (wet areas) na zisizohitaji maji |(dry areas), sehemu zenye kuhitaji nishati na kutoa nishati-hot areas na hivyo kurahisisha matumizi bora ya maji na nishati.Na katika zama hizi ambayo dunia inashuhudia uhaba wa maji na nishati katika nchi za Afrika,ni vizuri wasanifu majengo waanze kufikiria majengo ambayo ni rafiki katika matumizi na rafiki wa mazingira

10.Kwa nyumba ambazo ni za wakazi wengi,ni vema ikazingatia kukuza uhusiano na undugu mfano kuwe na kibaraza (verandah ya pamoja), sehemu za mapumziko za pamoja pia,ili kuhakikisha ujamaa na ushirikiano unadumishwa

 Kumbuka nyumba
utakayoijenga ni sehemu ya kudumu ( permanent structures) hivyo ni vizuri ukifahamu mapema mambo haya kabla ya kujenga kuepuka mkanganyiko wa kisaikolojia,maamuzi na uchumi. 
N:B- Nyakati hizi watu wanapenda nyumba ambazo zinaondoa kabisa uhusiano wa kijamii mfano
ukaribu na majirani,ushirikiano-nadhani ni wakati sasa wasanifu majengo Tanzania wafikirie ni jinsi gani kinachoitwa privacy kinavyoathiri ujamaa,enzi za nyerere fikra ilikuwa watu wanaotumia apartment wapike pamoja,wafue sehemu moja,lakini kwa sasa watanzania
wanafiki tofauti na labda kwa sababu hatuna falsafa inayoliunganisha taifa

CHANZO/HATIMILIKI YA STORI: UJENZIBORATZ

Kwa maswali na maoni Wasiliana nasi UJENZIBONGO ama wasiliana na UJENZIBORATZ kupitia anwani pepe nyumbaboratz@gmail.com

No comments: