• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Saturday, March 28, 2015

LUKUVI AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA ZA NHC ZA MAKAZI SUMBAWANGA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wa tatu kulia na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya wa kwanza kushoto wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba 20 za makazi zinazojengwa na Shirikia la Nyumba la Taifa (NHC) katikati ya Manispaa ya Sumbawanga tarehe 26/03/2015. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Ndugu Nehemia Mchechu nyumba hizo ambazo ni za ghorofa moja zitauzwa baada ya kukamilika ujenzi wake kwa njia ya fedha taslimu na njia ya Mikopo ya benki. 
Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi katikati akiweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa nyumba 20 za makazi zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa Mjini Sumbawanga kwa kushirikiana na viongozi wengine wa chama na Serikali Mkoani Rukwa tarehe 26/03/2015.
Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Ndugu Nehemia Mchechu katika hafla fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za makazi za shirika hilo Mjini Sumbawanga.
Michoro ya mradi huo. (Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa
picha zaidi >>Rukwareview.blogspot.com

Saturday, January 19, 2013

Umeshawahi kufikiria kuwa na sakafu ya mbao ndani ya nyumba yako?

DSCN7253Sakafu ya mbao, kitaalamu inaitwa “Parquet Flooring”. Sakafu hii kama picha inavyoonesha imeunganishwa na tiles zenye rangi inayofanania nazo
DSCN7263Hizi ni stepu za ngazi ambazo zimewekewa mbano ngumu badala ya tiles ama bidhaa nyingineyo. Iking’arishwa na varnish/polish hupendeza sana!
DSCN7275
DSCN7296Sakafu hii ni ya mbao tupu kabla ya kung’arishwa

External Pavings kwa kutumia mawe ya mtoni

DSCN7304Leo Blog yako ya ujenzi inakuletea teknolojia mpya ya kutengeneza madhari ya kuzunguka nyumba na kwa kutumia mawe madogomadogo yanyopatikana mtoni.

Kama picha inavyoonesha mawe haya madogo hupangwa kwa kuunganishwa karibu juu ya surface ngumu iliyoandaliwa maalumu, na baadae kukaziwa na mchanganyiko wa sementi na mchanga kwenye maunganiko. Haya hutumiak kama mbadala wa paving blocks, slabs, tiles ama screeding ya kawaida.
DSCN7249

Saturday, December 15, 2012

JK AZINDUA NYUMBA ZA BEI NAFUU ZA NHC KIBADA, KIGAMBONI,DAR

Rais Jakaya Kikwete (alivaa koti la rangi ya maziwa) akikagua moja kati nyumba 290 za bei nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) eneo la Kibada, Kigamboni Dar es Salaam Desemba 13,2012. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu.(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

JK akisalimiana na wafanyakazi wa NHC alipowasili kuzindua nyumba hizo

                                              Kikundi cha hamasa kikitumbuiza

JK akitoa maelezo kwa Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye wakati wa uzinduzi wa nyumba hizo.

                                    JK akiwa na baadhi ya maofisa wa NHC

Baadhi ya nyumba zilizozinduliwa  na Rais Kikwete











IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AKABIDHI NYUMBA MPYA 35 ZA WALIOATHIRIKA NA MILIPUKO YA MABOMU YA GONGO LA MBOTO JANA JIJINI DAR ES SALAAM



Picha juu ni Baadhi ya  nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto  katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekqana  leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete

kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa  kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto  katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012

Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiakata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga  nyumba mpya 35 kwa ajili ya  waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.Picha na IKULU







Saturday, December 8, 2012

MAONESHO YA NYUMBA YAANZA DAR

 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana (katikati) akikata utepe kuzindua rasmi maonesho ya Nyumba yaliyoandaliwa na Kampuni ya Tanzania Home Export
kwenye viwanja vya Mlimani City, Dar es Salaam kwa siku tatu kuanzia leo.Kushoto ni Mkurugenzi wa Matukio wa kampuni hiyo,Zeno Ngowi na Rhoda Furaha.

Baadhi nyumba za kuuzwa zinazojengwa na Kampuni ya Sea Breeze eneo la Jangwani, Mbezi Beach Dar es Salaam.

                                           Wananchi wakiangalia nyumba hizo


                                         Moja ya mabanda yaliyopo kwenye maonesho hayo

DC Rugimbana akisalimiana na  Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa  Benki ya Azania, Othman Jabrie alipotembelea banda hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana akitembelea banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)

Rugimbana akizungumza na Mkuu wa Fedha Mwandamizi wa TMRC, Oswald Urassa. (PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO – RICHARD MWAIKENDA)













Tuesday, October 23, 2012

Interior design for a hotel room

SAM_5933
SAM_5931

Monday, October 8, 2012

Taswira Za Ujenzi Wa Stendi Kuu Ya Mabasi Kigoma Unaendelea



Stendi hii itakuwa maeneo ya Masanga katika kata ya Gungu,Kigoma.
Picha na Iddy Allute,akiwa Kigoma, kupitia Mjengwa Blog

Taswira: Makamu wa Rais Dkt. Bilal Akihitimisha Matembezi ya Wahandisi jana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki katika matembezi ya hisani ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Matembezi hayo yalianzia katika Viwanja vya Karimjee jijini na kumalizikia katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Moahammed Gharib Bilal,akimkabidhi cheti, Mhandisi Grace Beo, kutoka Kampuni ya Temesa ICT Engineer, akiwa ni mmoja kati ya waliochangia na kushiriki vyema katika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Makamu alikabidhi vyeti hivyo baada ya kuhitimisha rasmi matembezi hayo ya hisani yaliyoanzia katika Viwanja vya Karimjee na kumalizikia kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na Wahandisi (Local Engineers) baada ya kuhitimisha matembezi hayo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Daar es Salaam leo, Oktoba 7, 2012.

Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

Wednesday, September 5, 2012

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI AZINDUA UJENZI WA JENGO KUU LA ELIMU HURIA NA MASAFA

Picha ya pamoja, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Shukuru Kawambwa pamoja na Mama Maria Nyerere aliyekuwepo katika uzinduzi huo.

Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kama linavyoonekana ambalo ujenzi wake umezinduliwa leo 5/9/2012 na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Kawambwa



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk.Kawambwa akifurahi baada ya kuzindua ujenzi wa Jengo kuu la Elimu Huria na Masafa leo huku Mama Maria Nyerere akimpongeza.

Mama Maria Nyerere,Mhe.Dk.Kawambwa wakifurahia jambo na wageni wengine baada ya uzinduzi  wa Jengo 

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,Prof.Tolly Mbwette akitoa maelezo ya awali kuhusiana na ujenzi wa Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kwa Wageni waalikwa katika uzinduzi waliokuja kushuhudia Uzinduzi huo leo 5/9/2012 katika Ofisi za Muda za Chuo Kinondoni,Dar es Salaam.
SOURCE: RUNDUGAI BLOG








ROOF CONSTRUCTION FOR RESIDENTIAL HOUSES

DSCN5202Kenji (truses) zikiwa zimeshikizwa kwenye bimu ya zege (reiforced concrete beam) kutengeneza paa la nyumba mtindo wa (pitch) kama linavyoonekana kwa kutokea ndani. Bolt na nati ndizo zimetumika kushikilia bimu zikikazwa kwa kucomewa (welding). Tie beam wametumia mbao mbili kwa uimara zaidi. Kwa kawaida kenji linaweza kuwa la chuma au mbao kutegemeana na uimara unaohitajika. Mbao za kenji zina ukubwa wa 150x50mm.

DSCN5230

Mbao ulalo kwa saizi ya unene wa 50x50mm zimewekwa kwa upana unaofanana. kwa kitaalamu mbao hizi huitwa purlins.

DSCN5209

Vigae hupangwa kimoja kimoja kwa kufuata purlins zilivyojipanga

DSCN5201