Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Ndugu Nehemia Mchechu katika hafla fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za makazi za shirika hilo Mjini Sumbawanga.-
Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?
Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.
-
Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?
Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.
-
Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?
Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.
Saturday, March 28, 2015
LUKUVI AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA ZA NHC ZA MAKAZI SUMBAWANGA
Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Ndugu Nehemia Mchechu katika hafla fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za makazi za shirika hilo Mjini Sumbawanga.Saturday, January 19, 2013
Umeshawahi kufikiria kuwa na sakafu ya mbao ndani ya nyumba yako?
External Pavings kwa kutumia mawe ya mtoni
Kama picha inavyoonesha mawe haya madogo hupangwa kwa kuunganishwa karibu juu ya surface ngumu iliyoandaliwa maalumu, na baadae kukaziwa na mchanganyiko wa sementi na mchanga kwenye maunganiko. Haya hutumiak kama mbadala wa paving blocks, slabs, tiles ama screeding ya kawaida.
Saturday, December 15, 2012
JK AZINDUA NYUMBA ZA BEI NAFUU ZA NHC KIBADA, KIGAMBONI,DAR
JK akisalimiana na wafanyakazi wa NHC alipowasili kuzindua nyumba hizo
Kikundi cha hamasa kikitumbuiza
JK akitoa maelezo kwa Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye wakati wa uzinduzi wa nyumba hizo.
JK akiwa na baadhi ya maofisa wa NHC
Baadhi ya nyumba zilizozinduliwa na Rais Kikwete
IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AKABIDHI NYUMBA MPYA 35 ZA WALIOATHIRIKA NA MILIPUKO YA MABOMU YA GONGO LA MBOTO JANA JIJINI DAR ES SALAAM
Picha juu ni Baadhi ya nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekqana leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete
kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012
Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiakata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga nyumba mpya 35 kwa ajili ya waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.Picha na IKULU
Saturday, December 8, 2012
MAONESHO YA NYUMBA YAANZA DAR
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana (katikati) akikata utepe kuzindua rasmi maonesho ya Nyumba yaliyoandaliwa na Kampuni ya Tanzania Home Export
kwenye viwanja vya Mlimani City, Dar es Salaam kwa siku tatu kuanzia leo.Kushoto ni Mkurugenzi wa Matukio wa kampuni hiyo,Zeno Ngowi na Rhoda Furaha.
Baadhi nyumba za kuuzwa zinazojengwa na Kampuni ya Sea Breeze eneo la Jangwani, Mbezi Beach Dar es Salaam.
Wananchi wakiangalia nyumba hizo
Moja ya mabanda yaliyopo kwenye maonesho hayo
DC Rugimbana akisalimiana na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Benki ya Azania, Othman Jabrie alipotembelea banda hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana akitembelea banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)
Rugimbana akizungumza na Mkuu wa Fedha Mwandamizi wa TMRC, Oswald Urassa. (PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO – RICHARD MWAIKENDA)
Tuesday, October 23, 2012
Monday, October 8, 2012
Taswira Za Ujenzi Wa Stendi Kuu Ya Mabasi Kigoma Unaendelea
Taswira: Makamu wa Rais Dkt. Bilal Akihitimisha Matembezi ya Wahandisi jana
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki katika matembezi ya hisani ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Matembezi hayo yalianzia katika Viwanja vya Karimjee jijini na kumalizikia katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Moahammed Gharib Bilal,akimkabidhi cheti, Mhandisi Grace Beo, kutoka Kampuni ya Temesa ICT Engineer, akiwa ni mmoja kati ya waliochangia na kushiriki vyema katika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Makamu alikabidhi vyeti hivyo baada ya kuhitimisha rasmi matembezi hayo ya hisani yaliyoanzia katika Viwanja vya Karimjee na kumalizikia kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na Wahandisi (Local Engineers) baada ya kuhitimisha matembezi hayo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Daar es Salaam leo, Oktoba 7, 2012.
Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais
Wednesday, September 5, 2012
WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI AZINDUA UJENZI WA JENGO KUU LA ELIMU HURIA NA MASAFA
Picha ya pamoja, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Shukuru Kawambwa pamoja na Mama Maria Nyerere aliyekuwepo katika uzinduzi huo.
Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kama linavyoonekana ambalo ujenzi wake umezinduliwa leo 5/9/2012 na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Kawambwa

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk.Kawambwa akifurahi baada ya kuzindua ujenzi wa Jengo kuu la Elimu Huria na Masafa leo huku Mama Maria Nyerere akimpongeza.
Mama Maria Nyerere,Mhe.Dk.Kawambwa wakifurahia jambo na wageni wengine baada ya uzinduzi wa Jengo
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,Prof.Tolly Mbwette akitoa maelezo ya awali kuhusiana na ujenzi wa Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kwa Wageni waalikwa katika uzinduzi waliokuja kushuhudia Uzinduzi huo leo 5/9/2012 katika Ofisi za Muda za Chuo Kinondoni,Dar es Salaam.
SOURCE: RUNDUGAI BLOG
ROOF CONSTRUCTION FOR RESIDENTIAL HOUSES
Kenji (truses) zikiwa zimeshikizwa kwenye bimu ya zege (reiforced concrete beam) kutengeneza paa la nyumba mtindo wa (pitch) kama linavyoonekana kwa kutokea ndani. Bolt na nati ndizo zimetumika kushikilia bimu zikikazwa kwa kucomewa (welding). Tie beam wametumia mbao mbili kwa uimara zaidi. Kwa kawaida kenji linaweza kuwa la chuma au mbao kutegemeana na uimara unaohitajika. Mbao za kenji zina ukubwa wa 150x50mm.
Mbao ulalo kwa saizi ya unene wa 50x50mm zimewekwa kwa upana unaofanana. kwa kitaalamu mbao hizi huitwa purlins.
Vigae hupangwa kimoja kimoja kwa kufuata purlins zilivyojipanga










