• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Saturday, December 15, 2012

JK AZINDUA NYUMBA ZA BEI NAFUU ZA NHC KIBADA, KIGAMBONI,DAR

Rais Jakaya Kikwete (alivaa koti la rangi ya maziwa) akikagua moja kati nyumba 290 za bei nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) eneo la Kibada, Kigamboni Dar es Salaam Desemba 13,2012. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu.(PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

JK akisalimiana na wafanyakazi wa NHC alipowasili kuzindua nyumba hizo

                                              Kikundi cha hamasa kikitumbuiza

JK akitoa maelezo kwa Mchechu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye wakati wa uzinduzi wa nyumba hizo.

                                    JK akiwa na baadhi ya maofisa wa NHC

Baadhi ya nyumba zilizozinduliwa  na Rais Kikwete











IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AKABIDHI NYUMBA MPYA 35 ZA WALIOATHIRIKA NA MILIPUKO YA MABOMU YA GONGO LA MBOTO JANA JIJINI DAR ES SALAAM



Picha juu ni Baadhi ya  nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto  katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekqana  leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete

kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa  kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto  katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012

Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiakata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga  nyumba mpya 35 kwa ajili ya  waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.Picha na IKULU







Saturday, December 8, 2012

MAONESHO YA NYUMBA YAANZA DAR

 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana (katikati) akikata utepe kuzindua rasmi maonesho ya Nyumba yaliyoandaliwa na Kampuni ya Tanzania Home Export
kwenye viwanja vya Mlimani City, Dar es Salaam kwa siku tatu kuanzia leo.Kushoto ni Mkurugenzi wa Matukio wa kampuni hiyo,Zeno Ngowi na Rhoda Furaha.

Baadhi nyumba za kuuzwa zinazojengwa na Kampuni ya Sea Breeze eneo la Jangwani, Mbezi Beach Dar es Salaam.

                                           Wananchi wakiangalia nyumba hizo


                                         Moja ya mabanda yaliyopo kwenye maonesho hayo

DC Rugimbana akisalimiana na  Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa  Benki ya Azania, Othman Jabrie alipotembelea banda hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana akitembelea banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)

Rugimbana akizungumza na Mkuu wa Fedha Mwandamizi wa TMRC, Oswald Urassa. (PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO – RICHARD MWAIKENDA)













Tuesday, October 23, 2012

Interior design for a hotel room

SAM_5933
SAM_5931

Monday, October 8, 2012

Taswira Za Ujenzi Wa Stendi Kuu Ya Mabasi Kigoma Unaendelea



Stendi hii itakuwa maeneo ya Masanga katika kata ya Gungu,Kigoma.
Picha na Iddy Allute,akiwa Kigoma, kupitia Mjengwa Blog

Taswira: Makamu wa Rais Dkt. Bilal Akihitimisha Matembezi ya Wahandisi jana

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki katika matembezi ya hisani ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Matembezi hayo yalianzia katika Viwanja vya Karimjee jijini na kumalizikia katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Moahammed Gharib Bilal,akimkabidhi cheti, Mhandisi Grace Beo, kutoka Kampuni ya Temesa ICT Engineer, akiwa ni mmoja kati ya waliochangia na kushiriki vyema katika zoezi la kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uwezo wa Wahandisi wa Tanzania, yaliyoandaliwa na Wahandisi hao (Local Engineers). Makamu alikabidhi vyeti hivyo baada ya kuhitimisha rasmi matembezi hayo ya hisani yaliyoanzia katika Viwanja vya Karimjee na kumalizikia kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na Wahandisi (Local Engineers) baada ya kuhitimisha matembezi hayo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni, jijini Daar es Salaam leo, Oktoba 7, 2012.

Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

Wednesday, September 5, 2012

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI AZINDUA UJENZI WA JENGO KUU LA ELIMU HURIA NA MASAFA

Picha ya pamoja, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Shukuru Kawambwa pamoja na Mama Maria Nyerere aliyekuwepo katika uzinduzi huo.

Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kama linavyoonekana ambalo ujenzi wake umezinduliwa leo 5/9/2012 na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Kawambwa



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk.Kawambwa akifurahi baada ya kuzindua ujenzi wa Jengo kuu la Elimu Huria na Masafa leo huku Mama Maria Nyerere akimpongeza.

Mama Maria Nyerere,Mhe.Dk.Kawambwa wakifurahia jambo na wageni wengine baada ya uzinduzi  wa Jengo 

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,Prof.Tolly Mbwette akitoa maelezo ya awali kuhusiana na ujenzi wa Jengo la kuu la Elimu Huria na Masafa kwa Wageni waalikwa katika uzinduzi waliokuja kushuhudia Uzinduzi huo leo 5/9/2012 katika Ofisi za Muda za Chuo Kinondoni,Dar es Salaam.
SOURCE: RUNDUGAI BLOG








ROOF CONSTRUCTION FOR RESIDENTIAL HOUSES

DSCN5202Kenji (truses) zikiwa zimeshikizwa kwenye bimu ya zege (reiforced concrete beam) kutengeneza paa la nyumba mtindo wa (pitch) kama linavyoonekana kwa kutokea ndani. Bolt na nati ndizo zimetumika kushikilia bimu zikikazwa kwa kucomewa (welding). Tie beam wametumia mbao mbili kwa uimara zaidi. Kwa kawaida kenji linaweza kuwa la chuma au mbao kutegemeana na uimara unaohitajika. Mbao za kenji zina ukubwa wa 150x50mm.

DSCN5230

Mbao ulalo kwa saizi ya unene wa 50x50mm zimewekwa kwa upana unaofanana. kwa kitaalamu mbao hizi huitwa purlins.

DSCN5209

Vigae hupangwa kimoja kimoja kwa kufuata purlins zilivyojipanga

DSCN5201

Monday, September 3, 2012

WAHANDISI KUADHIMISHA SIKU YAO MWEZI HUU, JIJINI DAR

Mhandisi Prof. Ninatubu Lema

Na Aron Msigwa – MAELEZO.

Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini Bodi ya Usajili wa Wahandisi nchini imewataka watanzania kutumia huduma za  wakandarasi waliosajiliwa kisheria ili kuepuka kupata maafa na hasara inayotokana na ujenzi hafifu usiokidhi viwango.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (jana)  jijini Dar es salaam mwenyekiti wa bodi hiyo Prof. Ninatubu Lema amesema  kuwa wakati umefika kwa watanzania kuwaamini wahandisi wa ndani kutokana na kazi nzuri zinazofanyika na  hatua kubwa iliyofikiwa katika utoaji wa huduma bora  za ushauri na ujenzi tofauti na kipindi kilichopita.

Amesema katika kuimarisha  na kuboresha huduma za ushauri na ujenzi  nchini Bodi ya Usajili wa Wahandisi nchini kwa kushirikiana na wadau wengine wa taasisi za kihandisi  pamoja na wale wa Jumuiya ya Kihandisi watakutana jijini Dar es salaam kwa lengo la kuoinyesha jamii kile ambacho wahandisi wa Kitanzania wanaweza kukifanya katika kuleta maendeleo nchini.

Ameeleza kuwa hivi sasa kuna wahandisi wengi wanaofanya shughuli za usimamizi wa miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu nchini ikiwemo miradi ya barabara , gesi na shughuli za uchimbaji wa madini pia wapo wahandisi wa kitanzania wanaofanya kazi za ushauri katika mataifa mbalimbali ndani na ne ya bara la Afrika.

‘’Kwa upande wetu Tanzania wakati tunapata uhuru tulikua na wahandisi 2 na sasa wako zaidi ya elfu kumi ,jambo hili ni kubwa kwa sababu mchango wa wahandisi sasa tunauona katika kuleta maendeleo ya taifa maana bila ya kuwa na wahandisi vitu vyote tunavyoviona kama barabara, majengo, na miundombinu mbalimbali haviwezi kuwepo”

Prof. Lema amesema maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini yanalenga kuwatambua wahandisi na makampuni  na mashirika ya Kihandisi yaliyotoa mchango mikubwa ya kihandisi katika maendeleo ya taifa na kuwahamasiha wahandisi wengine kufanya shughuli zao vizuri zaidi.

Ameongeza  kuwa maadhimisho yataambatana na tuzo mbalimbali zenye lengo la kuwatia Moyo wanafunzi wahitimu kutoka vyuo vikuu na Taasisi za Uhandisi nchini pamoja na taasisi zitakazotia fora kwenye maonyesho ya ufundi pia kuwafanya vijana washawishike kusomea taaluma ya uhandisi.

Kwa upande wake msajili wa Bodi ya Usajili wa wahandisi Eng. Steven Mlote akizungumzia kuhusu ubora wa majengo yanayoendelea kujengwa kwa wingi jijini Dar es salaam amesema kuwa wamiliki wa majengo hayo wanao mchango mkubwa katika kuhakikisha kuwa ujenzi wa majengo yao unazingatia viwango.

Amesema yeye kama msajili anawashauri wamiliki wa majengo kuhakikisha kuwa majengo yao yanayojengwa hivi sasa yanajengwa na wahandisi waliosajiliwa huku akitoa tahadhali kwa wale wanaokiuka kanuni zilizowekwa katika kusimamia ujenzi wa majengo nchini.

“Nawaomba wamiliki wote kuhakikisha kuwa pindi wanapoanza ujenzi wa majengo yao wahakikishe kuwa wanawatumia makandarasi waliosajiliwa, na mtu yeyote anayeruhusu jingo lake kujengwa na watu au kandarasi zisizosajiliwa anakiuka sheria na anastahili kushtakiwa” amebainisha Mlote.

Kwa upande wake Eng. Benedict. Mukama amewataka wananchi kutoa ushirikiano katika kuyabaini majengo yote yanayojengwa nchini chini ya viwango na kutoa taarifa kwa mamlaka husika ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya makandarasi wanaohusika na ujenzi wa miradi hiyo huku akieleza kuwa katika mwaka wa fedha 2011/2012 zaidi ya miradi 164 iliyokuwa inajengwa kinyume cha utaratibu bila kuzingatia viwango ikiwemo ya barabara imesimamishwa.

Aidha amesema maadhimisho haya ya siku ya wahandisi 2012 ambayo yanaadhimishwa nchini kwa mara ya 10 yatakuwa na mvuto wa pekee kwa kuwa yanawawahusisha washiriki kutoka kutoka nchi za Maziwa Makuu,Afrika ya Mashariki na zile za Jumuiya ya Maendeleo ya  kusini mwa Afrika (SADC).

Tuesday, February 28, 2012

LIST OF DELETED CONTRACTORS

The Contractors Registration Board wishes to inform all clients, Consultants and general public that the following contractors have been deleted from their Register of Contractors with effect from 01.01.2012 in accordance with subsection 13 (1) (b) (c) and (d) and 15 (1) (c) respectively of the Contractors Registration Act No. 17 of 1997 as amended by The Contractors Registration (Amendments) Act No. 15 of 2008. Find the list....

Monday, February 27, 2012

Ardhi University Set to Survey Gas Pipeline Route

THE Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) has engaged Ardhi University (ARU) to survey the route of the envisaged natural gas pipeline from Mnazi Bay in Mtwara Region to Dar es Salaam via Somanga, it has been learnt. For more information, just visit the source of information, the Daily News of 27th February, 2012.

Asbestos ni hatari kwa afya: Je, Wanafunzi hawa wako salama?

Asbestos ilitumika zaidi kama bidhaa ya ujenzi wa majumba kati ya miaka ya 1950 na 1970. Bidhaa hii ilipendwa zaidi kutokana na uwezo wake wa kutunza hali ya joto au ubaridi.
Kwa sasa karibia kila nchi duniani imekwishapiga marufuku matumizi ya bidhaa hii kutokana na atahri za kiafya zinazosababbishwa na vipande vidogo vidogo vya bidhaa hii kuingia kwenye mwili wa binadamu kwa mfumo wa hewa na kuleta madhara.

Nchini Tanzania pia bidhaa hii ilikwisha kupigwa marufuku kutumika na kiwanda chake kilichokuwepo pembezoni mwa kiwanda cha cement Wazo Hill, Dar es Salaam, njia ya Bagamoyo kilishafunga uzalishaji wa bidhaa hii.

Wataalamu wanatuambia kuwa bidhaa ya asbestos ina madhara zaidi ukiwa unaitoa kwenye paa tofauti na ukiwa unaiweka/unaiezeka kama inavyoelezwa humu. Inaelezwa pia hata uchakavu wa bidhaa hii kutokaka na kukaa muda mrefu na kuathiriwa na hali ya hewa, bado madhara yatokanayo na bidhaa hii ni makubwa kwa afya ya mwanadamu endapo itatokea akavuta chembechembe ndogo kwa njia ya hewa.

Mamlaka inayoshughulika na mazingira nchini,NEMC imeweka utaratibu maalumu wa kutumia wataalamu katika kuteketeza mabaki ya bidhaa za asbestos ili zisiweze kuleta madhara kwa binadamu nchini.

Pichani wanaonekana wanafunzi nje ya darasa ambalo limeezekwa kwa kutumia bidhaa hii ya asbestos ambayo imepigwa marufuku kutumika nchini na sehemu nyingine duniani. Hii ni shule mpya ya Suye, ipo Jijini Arusha (shule ya Kata) na ndio imeanza wiki chache zilizopita. Jengo hili la darasa ni chumba ambacho hapo awali kilikuwa ni chumba cha kiwanda cha matofali. Kutokana na uhaba wa nafasi za watoto kuweza kusoma, Serikali ikaamua kuyabadilisha majengo hayo ili yapatikane madarasa kwa ajili ya kuwapokea wananfunzi hawa wa kidato cha kwanza. Sitaki kuamini wataalamu wa ujenzi walioshirikishwa hawakuona hatari ya kuwaweka watoto nadani ya mabati haya ambayo pasi na shaka yamekwishachakaa sana na uwezekano wa sumu kutoka ni mkubwa sana.

Hata hivyo, kitaalamu zipo namna za kuweza kuzuia madhara bila kuyaezua mabati haya. Ni zoezi ambalo linagharimu fedha kiasi. Lakini kwa hii shule, japo sio madarasa yote yana hii biidhaa, bado hakuna dalili za uwezekano kuwa kuna tahadhari yeyote imechukuliwa kudhibiti madhara ya sumu ya asbetos isiweze kuwadhuru wanafunzi hawa. Afya za watoto hawa ziko salama kiasi gani!?

Friday, February 24, 2012

Designer wetu wa leo..


Hii ni moja ya design iliyofanywa na vijana wa kitanzania. Ni mfano wa makazi bora kwa mwanadamu hasa katika ulimwengu huu wa sasa wa maendeleo ya kiteknolojia...
Mhusika wa kazi hii ni Masunga Matondo ambae ni Achitect/Designer na unaweza kutembelea ukurasa wake wa Facebook kwa kupitia kwa link hiyo ya jina lake moja kwa moja. Tupende kutumia vyakwetu na wataalamu wetu.

Blog hii itakuletea kazi nyingi za kijana huyu mwenye kipaji cha ubunifu wa kipekee.

Announcement: Contractors Training Course on 27th February 2012

The Contractors Registration Board (of Tanzania)informs all Contractors that the training couse of FINANCIAL MANAGEMENT (Module SC 170/MC 290) will take place at the ASA Hall, Dar es Salaam Institute of Technology starting at 8:30 am on Monday 27th February 2012.

The fees for the course is TShs 200,000/= per person for Registered Contractors.

Other cources for Contractors and other construction industry practitioners under SSTP Programme for 2012 are scheduled to happen as follows..
Kigoma 26th-30th March 2012
Arusha 16th-20th April 2012
Iringa 30th July-3rd August 2012
Dar es Salaam 27th-28th September 2012
Lindi 24th-28th September 2012.


For more details please visit the Contractors Registration Board's official website

Friday, February 10, 2012

APPOINTMENT OF A REGISTRAR - AQRB

The Board of Directors of Architects and Quantity Surveyors Registration Board (Under Act No. 4 of 2010) has appointed ARCH. JEHAD ABDALLAH JEHAD as a Registrar of the Board on Contract for five years with effects from 1st February 2012.

Tuesday, February 7, 2012

Maisha marefu katika nyumba bora...


Binadamau ni mmoja kati ya viumbe hai ambae hupenda kukaa mahali akajisikia raha. Afya ya binadamu huyu hutegemeana na mazingira anayoishi hususani mahali anapolala. Nyumba bora kwa viwango stahili huakisi afya bora kwa mtumiaji!

Nyumba kama hii inayoonekana pichani haiwezi kutoa uhakika wa afya ya aneishi kwa msingi kwamba vumbi pekee linatosha kusababisha athari za kiafya kwa watumiaji! Nyumba kama hizi yafaa sasa zibaki kama historia ya kizazi chetu kilipotoka, tuanze kuwazia nyumba bora kwa nchi nzimaWakulima na wafugaji vijijini ndio wanaonekana kuishi kwenye makazi duni zaidi kwasababu ya tabia yao ya kuhamahama.