• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Tuesday, February 28, 2012

LIST OF DELETED CONTRACTORS

The Contractors Registration Board wishes to inform all clients, Consultants and general public that the following contractors have been deleted from their Register of Contractors with effect from 01.01.2012 in accordance with subsection 13 (1) (b) (c) and (d) and 15 (1) (c) respectively of the Contractors Registration Act No. 17 of 1997 as amended by The Contractors Registration (Amendments) Act No. 15 of 2008. Find the list....

Monday, February 27, 2012

Ardhi University Set to Survey Gas Pipeline Route

THE Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) has engaged Ardhi University (ARU) to survey the route of the envisaged natural gas pipeline from Mnazi Bay in Mtwara Region to Dar es Salaam via Somanga, it has been learnt. For more information, just visit the source of information, the Daily News of 27th February, 2012.

Asbestos ni hatari kwa afya: Je, Wanafunzi hawa wako salama?

Asbestos ilitumika zaidi kama bidhaa ya ujenzi wa majumba kati ya miaka ya 1950 na 1970. Bidhaa hii ilipendwa zaidi kutokana na uwezo wake wa kutunza hali ya joto au ubaridi.
Kwa sasa karibia kila nchi duniani imekwishapiga marufuku matumizi ya bidhaa hii kutokana na atahri za kiafya zinazosababbishwa na vipande vidogo vidogo vya bidhaa hii kuingia kwenye mwili wa binadamu kwa mfumo wa hewa na kuleta madhara.

Nchini Tanzania pia bidhaa hii ilikwisha kupigwa marufuku kutumika na kiwanda chake kilichokuwepo pembezoni mwa kiwanda cha cement Wazo Hill, Dar es Salaam, njia ya Bagamoyo kilishafunga uzalishaji wa bidhaa hii.

Wataalamu wanatuambia kuwa bidhaa ya asbestos ina madhara zaidi ukiwa unaitoa kwenye paa tofauti na ukiwa unaiweka/unaiezeka kama inavyoelezwa humu. Inaelezwa pia hata uchakavu wa bidhaa hii kutokaka na kukaa muda mrefu na kuathiriwa na hali ya hewa, bado madhara yatokanayo na bidhaa hii ni makubwa kwa afya ya mwanadamu endapo itatokea akavuta chembechembe ndogo kwa njia ya hewa.

Mamlaka inayoshughulika na mazingira nchini,NEMC imeweka utaratibu maalumu wa kutumia wataalamu katika kuteketeza mabaki ya bidhaa za asbestos ili zisiweze kuleta madhara kwa binadamu nchini.

Pichani wanaonekana wanafunzi nje ya darasa ambalo limeezekwa kwa kutumia bidhaa hii ya asbestos ambayo imepigwa marufuku kutumika nchini na sehemu nyingine duniani. Hii ni shule mpya ya Suye, ipo Jijini Arusha (shule ya Kata) na ndio imeanza wiki chache zilizopita. Jengo hili la darasa ni chumba ambacho hapo awali kilikuwa ni chumba cha kiwanda cha matofali. Kutokana na uhaba wa nafasi za watoto kuweza kusoma, Serikali ikaamua kuyabadilisha majengo hayo ili yapatikane madarasa kwa ajili ya kuwapokea wananfunzi hawa wa kidato cha kwanza. Sitaki kuamini wataalamu wa ujenzi walioshirikishwa hawakuona hatari ya kuwaweka watoto nadani ya mabati haya ambayo pasi na shaka yamekwishachakaa sana na uwezekano wa sumu kutoka ni mkubwa sana.

Hata hivyo, kitaalamu zipo namna za kuweza kuzuia madhara bila kuyaezua mabati haya. Ni zoezi ambalo linagharimu fedha kiasi. Lakini kwa hii shule, japo sio madarasa yote yana hii biidhaa, bado hakuna dalili za uwezekano kuwa kuna tahadhari yeyote imechukuliwa kudhibiti madhara ya sumu ya asbetos isiweze kuwadhuru wanafunzi hawa. Afya za watoto hawa ziko salama kiasi gani!?

Friday, February 24, 2012

Designer wetu wa leo..


Hii ni moja ya design iliyofanywa na vijana wa kitanzania. Ni mfano wa makazi bora kwa mwanadamu hasa katika ulimwengu huu wa sasa wa maendeleo ya kiteknolojia...
Mhusika wa kazi hii ni Masunga Matondo ambae ni Achitect/Designer na unaweza kutembelea ukurasa wake wa Facebook kwa kupitia kwa link hiyo ya jina lake moja kwa moja. Tupende kutumia vyakwetu na wataalamu wetu.

Blog hii itakuletea kazi nyingi za kijana huyu mwenye kipaji cha ubunifu wa kipekee.

Announcement: Contractors Training Course on 27th February 2012

The Contractors Registration Board (of Tanzania)informs all Contractors that the training couse of FINANCIAL MANAGEMENT (Module SC 170/MC 290) will take place at the ASA Hall, Dar es Salaam Institute of Technology starting at 8:30 am on Monday 27th February 2012.

The fees for the course is TShs 200,000/= per person for Registered Contractors.

Other cources for Contractors and other construction industry practitioners under SSTP Programme for 2012 are scheduled to happen as follows..
Kigoma 26th-30th March 2012
Arusha 16th-20th April 2012
Iringa 30th July-3rd August 2012
Dar es Salaam 27th-28th September 2012
Lindi 24th-28th September 2012.


For more details please visit the Contractors Registration Board's official website

Friday, February 10, 2012

APPOINTMENT OF A REGISTRAR - AQRB

The Board of Directors of Architects and Quantity Surveyors Registration Board (Under Act No. 4 of 2010) has appointed ARCH. JEHAD ABDALLAH JEHAD as a Registrar of the Board on Contract for five years with effects from 1st February 2012.

Tuesday, February 7, 2012

Maisha marefu katika nyumba bora...


Binadamau ni mmoja kati ya viumbe hai ambae hupenda kukaa mahali akajisikia raha. Afya ya binadamu huyu hutegemeana na mazingira anayoishi hususani mahali anapolala. Nyumba bora kwa viwango stahili huakisi afya bora kwa mtumiaji!

Nyumba kama hii inayoonekana pichani haiwezi kutoa uhakika wa afya ya aneishi kwa msingi kwamba vumbi pekee linatosha kusababisha athari za kiafya kwa watumiaji! Nyumba kama hizi yafaa sasa zibaki kama historia ya kizazi chetu kilipotoka, tuanze kuwazia nyumba bora kwa nchi nzimaWakulima na wafugaji vijijini ndio wanaonekana kuishi kwenye makazi duni zaidi kwasababu ya tabia yao ya kuhamahama.