• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Thursday, February 22, 2018

Unahifadhi vipi saruji yako?


Simenti au saruji inahitajika kuhifadhiwa mahali palipo pakavu, pasiporuhusu unyevunyevu kupita kadiri iwezekanavyo. Na inashauriwa kama zimewekwa ndani ya nyumba basi mifuko yake ipangwe juu ya kichanja cha mbao na isigusane na ukuta kukwepa ubaridi wa sakafu na ukuta. Kukia na madirisha ya wastani itapendeza zaidi!

Si vyema sana kupanga mstari mmoja zaidi ya mifuko 10 mmoja juu ya mwingine. Zipange katika mtindo kwamba iliyotangulia kuhifadhiwa ndio itakayotumika kwanza kwa sababu ni rahisi sana saruji kuanza kuganda ikipata unyevunyevu. Kumbuka moja ya kipimo cha kujua ubora wa simenti ni ulaini vidoleni na kukosekana mabonge bonge yaliyoganda. 


Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N? Soma hapa kujua ubora tofauti wa simenti




Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu. 

Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi. Kwa baadhi ya nchi wana simenti ya uimara wa juu zaidi ya kipimo cha 52.5.

Kwa ujumla simenti hutumika kwa kutengenezea matofali, kuteneneza plaster na chipping, kusakafia, kuziba cracks, kuunganishia matofali kutengeneza ukuta, kutengenezea zege nk. 

Si ajabu ukaenda dukani na kunua saruji ya OPC ikiwa na mifuko yenye maandishi ya ubora kama 32.5N, 32.5R, 42.5N, 42.5R au hata 52.5N. Hizi herufi ‘N’ au ‘R’ hazina maana yeyote zaidi ya kuelezea kipindi cha mapema zaidi (umri) kwa simenti kuanza kufikia ubora wake ukipimwa katika siku 2 au 7.

Ni bahati nzuri Tanzania sasa ina viwanda vingi vya kuzalisha portland cement ambavyo hutambulika kwa majina kama Twiga Cement, Simba Cement, Tembo Cement, Moshi Cement, Dangote Cement n.k. WIngi huu wa wazalishaji huleta nafuu kwa walaji kupitia ushindani wa soko kibiashara.  

Tabia moja ya zege (mchanganyiko wa kokoto, mchanga na simenti katika uwioano uliopimwa na kuchanganywa na maji) huendelee kuwa bora kadiri siku zinavyoongezeka. Katika upimaji product ya zege, ubora hupimwa baada ya siku saba kuona kama kuna uwezekanao wa kufikia ubora unaotarajiwa huko baadae. Kipimo cha siku saba kikionesha kutoatoa majibu ya mwelekeo mzuri basi zege husika inabomolewa. Halafu kuna kipimo baada ya umri wa siku 14 na baadae siku 28 kuhitimisha kwamba viwango vya ubora vitafikiwa kadiri umri wa zege unavyoongezeka.  

Karibu tena Tujifunze!

WAKANDARASI WASIO WAZALENDO WASIPEWE KAZI NDANI YA JIJI LA DAR - NAIBU WAZIRI AWESO


Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea miundo mbinu ya maji safi na maji taka iliyopo katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi amemshukuru Naibu Waziri Aweso kwa msikamano ambao amekuwa akiufanya na wilaya yake ya kuwapa kipaumbele cha kuwatembelea mara kwa mara hali inayoamsha maendeleo zaidi.
Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASCO, Injinia Aron Joseph amewaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu kwa vile kwasasa wamejipanga zaidi kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa walio pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akiwa na mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi wakati alipofanya ziara ya kukagua miundo mbinu ya  maji kwa jiji la Dar es Salaam ambapo amejionea maendeleo mbali mbali ya ujenzi. Pichani akiwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya alipoanzia ziara hiyo.
Akikagua mradi wa Maji Taka (DEWAT) - Mlalakuwa.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akikagua mradi wa maji eneo la Makongo.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akipewa maelezo machache na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi wakati Waziri Awezo alipofanya ziara ya mradi wa maji eneo la Makongo juu ambapo ujenzi bado unaendelea.
Viongozi wa DAWASA, DAWASA pamoja na uomgozi wa serikali ya kijiji wakimsikiliza Naibu Waziri Aweso.
Wakitoka kukagua mradi wa ujenzi wa makongo juu.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi akisalimiana na Meneja wa DAWASCO-Kimara, Peter Fumbuka. Ambapo aliweza kumshukuru na kumpongeza kwa utendaji kazi wake na kumuomba achape kazi kwa bidii.
Muonekani wa ujenzi tanki la maji Makongo juu.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akiongea na mmoja ya wafanyakazi wa ujenzi wa mradi huo. Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG- DAR. Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso amewataka wakandarasi walio wazembe wasipewe kazi kwa  vile wamekuwa wakirudisha nyuma maendeleo kwa kuwakosesha wananchi kupata maji kwa wakati. Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati akifanya ziara katika wilaya ya Kinondoni ili kujionea ujenzi mbali mbali ya miundo mbinu inayoendeshwa na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) na Shirika la majisafi na majitaka jijini Dar es salaam (DAWASCO). Naibu Waziri Aweso amesema kuwa wakati umefika kwa wale wakandarasi wazembe kuacha kuchezea kazi wanazopewa, wafanye kazi kwa bidii ili huduma za maji zitolewe kwa wakati. "Nawaomba sana wale wakandarasi wazembe waache kuwepewa kazi maana wanachafua wilaya ya Kinondoni na Tanzania kwa ujumla maana nimetembelea miradi mbali mbali nimejionea uzembe unaofanywa na wakandarasi, ukiangalia mkandarasi kapewa hela asilimia 70 ila kazi aliyofanya ya asilimia 40 hii haikubaliki kabisa. Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi amemshukuru Naibu Waziri Aweso kwa msikamano ambao amekuwa akiufanya na wilaya yake ya kuwapa kipaumbele cha kuwatembelea mara kwa mara hali inayoamsha maendeleo zaidi. "Mimi sina mengi nitatekeleza maelekezo yote ambayo ameyatoa na nitakuwa msitari wa mbele kutoa maamuzi ya kina kwa wale makandarasi wazembe, sitamuonea aibu mtu,' amesema Naibu Waziri Aweso. Nae Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASCO, Injinia Aron Joseph amewaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu kwa vile kwasasa wamejipanga zaidi kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa walio pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam. "Tunamalizia ujenzi wa matanki makubwa ambayo tutaweza kuwasambazia wananchi wengi zaidi maji hasa walioko pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam," amesema Injinia Aron.