• Unataka Kujenga Ukuta Imara wa Nyumba Yako Utakaodumu Muda Mrefu?

    Ukuta wa nyumba ni sehemu muhimu na ya kudumu katika jengo lolote. Huweka uimara wa jengo na kudhibiti joto la nje na la ndani sambamba na kuweka usiri wa vitu vilivyomo ndani ya jingo. Hutoa ulinzi na kuweka usalma dhidi ya matukio ya hatari na wizi kwa vitu ama watu waliomo ndani.

  • Tunakosa nini Tusipotumia Wataalamu katika Ujenzi Wetu?

    Kushirikisha wataalamu kunatoa fursa ya kujua mbinu mpya na bora za ujenzi, kufaahamu vifaa vya ujenzi na sifa zake, kujua namna ya kupata gharama nafuu za ujenzi na usanifu majengo kuendana na ndoto yako binafsi.

  • Unafahamu Nini Ukinunua Simenti Imeandikwa 32.5N au 42.5N?

    Kuna madaraja matatu ya ubora/uimara wa simenti/saruji ambayo ni uimara wa chini 32.5, uimara bora zaidi ya ule wa chini 42.5 na uimara wa juu zaidi 52.5. Saruji ya gredi 52.5 bado haijaanza kuzalishwa kwa soko la Tanzania. Hii ni kusema kwamba tuna gredi ya 32.5 na 42.5 tu.Simenti ya daraja la chini la ubora 32.5 inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo, na ile ya daraja la juu zaidi yani 42.5 inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Saturday, December 31, 2016

Fahamu Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Ukichagua Ramani ya Nyumba Ili Usijutie Baadae

Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Ukichagua Ramani ya Nyumba Ili Usijutie Baadae

UjenziBongo


1.   Usiwe mgeni kabisa kabisa kwa kilakitu kwenye michoro ya ujenzi. Hii itakusaidia kutomuachia fundi kila kitu yakiwemo matamanio yako binafsi yafanywe na yeye, yani awaze kwa niaba yako. Angalau uwe na ufahamu mdogo waudadisi wa baadhi ya vitu kama milango, madirisha,korido, vyumba, baraza n.k ili muweze kushauriana vizurinafundi au mbunifu mpakaupate kile roho yako inataka.

2.       Fikiria maisha yako halisi na aina ya familiauliyo nayo na mtakavyoishi kwenye nyumba. Hapa namaanishalifestyle yenu. Kamaweusichague ramani tu kwa kudhani kila ramani inaendanana staili ya maisha ya kila mtu. Life style za maisha yetu hutofautiana. Unaweza kuwa unapendanyumba ya gorofa mwingine hapaendi au wewe unataka nyumba iliyojitanua chini na kona nyingi mwingine hataki.

UjenziBongo

3.       Fikiria idadi ya vyumba na nafasi unavyohitaji kulinganana ukubwa wa familia yako sasa na baadae. Jaribu kuwaza kama ndio unaishi ndani; chumba gani kiwe wapi nauweke nini, sebule iweje nauhusiano wake na jiko,dinning uwe namna gani,na mambo mengine kama hayo. Wakati mwingine kuokoa gharamakama za mfumo wa maji safi na maji taka ni muhimu kujua maeneo kama jiko, bafu na vyoo vinakaa maeneo gani.

4.       Hakikishaunadhibiti matamanio ya urembo mwingi (Architectural beauty) ili kupunguza gharamazisizo za lazima baadae. Sio kilaurembo unaouona kwa jirani ndio pekee unafaa kwako. Unaweza kushauriana na mtaalamu na kubuni features zako binafsi na nafuu. Epuka kuweka urembo ambaoutasababisha uwe na maintenance cost kubwa baadae.


UjenziBongo



5.       Hakikisha ukubwa wa rumu, korido, sebule, jiko, veranda,bafu na choo n.k aina ya fenicha na samani ulizonazoau utakazonunua kwa mahitaji yako na familia. Usingojee nyumba ikajengwa tayari ndio uanze kujaribisha vitu kama vinatoshea. Kama unatamani kitanda kikubwa hakikisha mapema kabisa ramani yako inaruhusu hilo na kuacha nafasi kiasi ya kujimwayamwaya.

6.       Kawaida nyumba huwa inapendeza na kuvutia kukaa ndani ikiwa na nafsi tofauti na kuwa imesongamana vitu kama vile ni stoo ya bidhaa. Kama wewe ni mtu wa burudani na kujumuika na marafiki nyumbani nyakati fulani fulani unaweza kuwaza kama vile yale maeneo muhimu kwa wageni wako yamejaa wakati wa kubuni ramani.

7.       Usalama ni jambo la muhimu kwako nafamilia. Nyumba yeyote lazima ikidhi mahitaji ya kiusalamakwa jingo lenyewena usalama wa matumizi na watuamiaji wake. Kuna masuala ya usalama ambayo yatasimamiwa na wataalamu,hayoni ya kiufundi Zaidi, muhimu ni kuwasisitiza yazingatiwe. Lakini pia kuna maswalaya usalama ya ninyi watuamiaji wa jingo na Zaidi watoto. Ni muhimu kujiridhisha vitu kama ngazi na reli zake, rail ya kwenye viambata, aina ya sakafu na vitu vingine ni salama kwa watumiaji na watoto hawatadhurika kwa aina ya michezo yao ilivyo.


UjenziBongo


8.       Tayari umeridhika na muonekano wa ndani na mgawanyo wavyumba, je, muonekano wan je naouakuvutia!? Kumbukama mahaliulipoamua chumba Fulani kikae,nyumba ikishajengwa huwezi kubadilishakwa mfano inatokea kwa ndani unapenda ukuta Fulani uwe na dirisha lakini kwanje unakuta dirisha likikaa hapo linaharibu umaridadi ulioutamani. Haya pia ni ya kuzingatia mwanzonikabisa kuendana na madhari ya mtaa unaoishi.

9.       Ankara. Chagua ramani na muundo sambamba na madoidoyake vinavyoendana na bajeti yako. Kama unawazia nyumba kubwa na bajeti haitoshi kukamilisha yote sasa unaweza kufikiria namnaya kupata ramani nzuri ambayo utaiendeleza taratibu huku ukiwaumehamiasehemumoja ya nyumba. Kupanga bajetinisoma jingine ambalonimeshalizungumzia kwenye Makala zilizopita.

10.   Ikiwezekana washirikishe wanafamilia wengine kuamua na kutoa ushauri kwa aina ya nyumba wanayoitamania pia. Kupitia mawazo yao unaweza kupatakilicho bora Zaidi badala yakilakitukuwa surprise tu. Mara nyingi huwa baba na mama ndiohushirikishana zaidikuamua, kama watotoni wakubwa si vibaya nao wakishirikishwa kwasababu kwa dunia ya sasa vyumba vya watotonavyo vina mahitaji yake binafsi. Ni vyemapia kujipa wakati na kupitia majarida tofauti tofauti na kujionea sampuli anuani kabla yakufikia hitimisho.



UjenziBongo
Maandaliziya materilasza ujenzi


UjenziBongo
Mafundi wakipaua nyumba,haa wanatengeneza kenji kwa ajili ya kubebea bati


KWA MAHITAJI YAKO YA USHAURI, RAMANI, WATAALAMU WA UJENZI NA UFUNZI WA AINA ZOTE USUSITE KUWASILIANA NASI KWA NAMBARI 0757718080 TUPO MOSHONO ARUSHA

Friday, December 23, 2016

Tile Flooring: Porcelain or Ceramic Tiles? Zijue tofauti hapa


Linapokuja suala la kufanya finishing ya nyumba yako unahitaji kufanya uamuzi wa aina gani ya materials utatumia kufanya finishing ya sakafu yako. Flooring (finishing ya sakafu) ziko za namna nyingi kutegemeana na materials utakayotumia kama vile VINYL, TILE,CARPET, NATURAL STONE, HARD WOOD, BAMBOO, AREA RUGS, LAMINATE na CEMENT & SAND SCREED. 

Ikumbukwe kwamba aina ya sakafu utakayochagua ina mchango mkubwa sana katika muonekano mzuri wa jengo lako. Muonekano mzuri wa jengo unatoa picha sahihi ya thamani ya jengo na kamanila biashara ya upangaji litavutia wateja zaidi. Hata hivyo sio wajenzi wote wanaweza kuchagua aina gani sahihi ya sakafu itafaa kwa majengo yao. Naomba nikupitishe taratibu kwenye makala ya leo, kwa kuanza tuangalie zaidi sakafu ya marumaru au vigae 'tile flooring'.  

Kama umeamua kutumia tiles kwenye jengo lako unalazimika kufahamu ni tiles gani utumie.  Hapo linaibuka swala la ama Marble, Ceramic tiles au Porcelain tiles. Kwa marble tiles tutaipangia toleo laken na kuijadili. Tuziangalie ceramic na porcelain tiles ambazo watu wengi na hata baadhi ya wauzaji huchukulia kama ni tiles aina moja. Kuna tofauti kidogo.

Kimsingi Porcelain na Ceramic tiles zote ni jamii moja ya tiles. Porcelain ni zao la ceramic kwa maanaya kwamba moja ni porcelain na nyingine ni non-porcelain. Sio rahisi kuzitofautisha kwa macholakini zina utofauti wa kitaalamu kwa namna zinavyotengenezwa na matumizi yake. Ieleweke kwamba bidhaa za porcelain zinapatikanakwenye vikombe, sahani n.k,hizi tunazoita sahani za udongo. Leo nitaeleza kwa ufupi kuhusu ceramic na porcelain tiles. Tusameheane pale ambapo nitashindwa kutumia nenola Kiswahili. 


Ceramic tiles ni mchanganyiko wa udongo maalumu (clay) na mchanganyiko mwingine asili. Porcelain tiles zenyewe zinatokana pia na udongo wa 'porcelain clay' lakini ni wa chembechembe ndogo sana ambazo zinachomwa kwa joto kali mno kiasi cha kufanya kaigae chake kiwe kigumu, kizito nahakipitishi maji kirahisi nahivyo kufaa kwa matumizi ya mazingira ya nje zaidi ya Ceramic tiles.

Katika kuzitofautisha kuna vitu vichache vya kufahamu ambavyo vinaweza kuwa muongozo sahihi kwako; kwamba 
  1. Ceramic tiles sioimara nazakudumu sana kwa matumizi ya nje ya jengo kwasababu zina tabia ya kunyonya sana maji kutokana na zilivyotengenezwa kwamba ninyepesina zina nafasi ya kuruhusu maji kupenya kwa urahisi. Kwa matumiziya nje hupelekea cracks baada ya muda fulanihasa kwa maeneo yenye unyevunyevu sana. 
  2. Porcelain tiles zinafaa zaidi kwa matumizi ya nje kwasababu yana kiwango kidogo cha kuruhusu maji kunyonywa nazo
  3. Porcelain tiles ni nzitozaidi na hazina nafasi wazi kuruhusu unyevunyevu kupenya kama Ceramic tiles na hivyo ni ngumu na nzito kubeba
  4. Porcelain zinadumu zaidi na zinafaa kwa maeneo ambayo ni yakupitika pitikana uzito mwingi
  5. Ceramic tiles ni laini sana kuzikata kulikoPorcelain tiles (huwazinakatwa kwakutumiamashine zinaitwa (Snap tile cutter au Wet tile saw)
  6. Na mwisho, ceramic tiles nafuu zaidi kwa maanaya gharama za kununua kuliko porcelain tiles














.

Wednesday, December 21, 2016

JE, UNAFAHAMU KUWA UBUNIFU WA JENGO HUAKISI GHARAMA HALISI ?

ujenziBongo.Co.Tz
Kitaalamu. ubunifu wa majengo hufanywa na wataalamu wanaitwa Architects ama kwa kiswahihi wabunifu majengo.

Ubunifu wa jengo ni hali ya kuumba taswira ya kufikirika na kuiweka katika hali  ya mwonekano wa kama kitu halisi, kwamba endapo ujenzi ukifanyika jengo litakuwa namna hiyo.

Ubunifu huwa ni hatua ya awali kabisa kwenye ujenzi kwa mtu ambaye tayari ana kiwanja chake na huwasilishwa kwa njia ya michoro ya kisanifu kama nilivyoeleza hapo juu, kwa kuchukua mawazo na matamanio ya mwenye kutaka kujenga na kuyaweka katika mpangiliowa mahitaji halisi kwa kuzingatia eneola ardhi lilivyo na ukubwa wake bila kusahau mazingira yanayozunguka eneohilo


Baadae utahitaji kujua gharama halisi za nyumba ya ndoto yako kulingana na ubunifu huo kwa bei ya sokoya wakatihuo. Pengine yawezekanaunahitaji kujenga baadae, nayoni sahihi kuwana mchoro na kujiandaa nao.

Hatua hii ningumukidogo na inahitaji uwe mwenye nidhamu sana katika kufikia malengo yako. Yawezekana pia umepata hela za mara moja kutokana na msihemishe zako na ukatamani ufanye uwekezaji wa nyumba. Ili kuepuka kuishia katikati ya safari, ni muhimu ukashirikisha wataalamu wabunifu na wakadiriaji gharama za ujenzi wakakushauri ni jengo gani na la ukubwa gani litatoshea pesa uliyo nayo kwamtindogani.

Kama kichwa cha habari cha somo kinavyoeleza, ubunifu ambao hutoa mwonekano halisi wa nyumba yako hutafsiri gharama halisi ya nyumba yako. Zipo njia mbalimbali zinazoweza kutumika kusaidia kupunguza gharama kwenye ujenzi na wakati huohuo ukaweza kupata jengo lamuonekano wa nyumba uitakayo. Watu wengi huwa wanajenga tu kwa mazoeana kuiganyumba za majirani, hawajisumbui kufanya ubunifu wa kile ambacho nafasi zao hutamani kuwa nazo. Unaweza kusoma baadhi ya mbinu hapa za kupunguza gharama

Hata hivyo, katika hatua ya ubunifu,zipo namnatofauti zakuweza kushauriana na mbunifu majengo na kuweza ya kupunguza gharama kwa kuondoa baadhi ya mahitaji yasiyo ya lazima, kwa mfano, kupunguza idadi ya kuta za ndani, kutokuwana nafasi nyingi zisizona ulaziman.k

Kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu, unaweza kujenga nyumba bora na ya kisasa, nyumba bora ndogo inayokidhi mahitaji naukaimaliza badala ya kujenga nyumba kubwa kwa mazoea na ukashindwa kuimaliza. Amua! Unaweza! 


Njia 13 za kuweza Kuokoa Gharama Ukijenga Nyumba


Leo nakusogezea dondoo chache zinazoweka kukusaidia kupunguza gharama wakati unaanza mchakato na kufanikishaujenzi wa jengolakolakuishi
1. Nunua eneo kwa ushirikiano na ndugu, jamaa na marafiki ambao mnaaminiana, mtu mnayeweza kuishi kama majirani na kuweza kugawana eneo/kiwanja husika. 

2. Tafuta eneo ambalo halikimbiliwi na watu wengi, eneoambalo walio wengi hawafikirii kununua. Usifikirie sana kununua maeneo ya pembezoni mwa bahari, tafuta maeneo mengine yaliyotengwa kwa makazi ilikuepuka kujenga mahali pasipostahili. Viwanja vya ufukweni huwana gharamakubwa sana

3. Nunua 'material' bora lakini ya gharama nafuu kufanikisha ujenzi wako. Usinunue tu kwasababu umeona aukusikia mwingine amenunua.

4. Unaweza kukusanya mabaki ya takataka za majengo yaliyobomolewa mahali,matofali yaliyotumika n.k yatakufaa mahali katika zoezizima la ujenzi. 

5. Fikiria zaidi vitu muhimu ambavyo una hakika huwezi kuishi bila kuwa navyo. Mfano, madirisha na milango ni muhimu kwa usalama lakini jaribu kuangalia bajeti yako inatoshea nini.

6. Usijenge nyumba kubwa sana kuzidi mahitaji yako na kwa kuangalia aina ya nyumba zilizozunguka eneo lako kwasababu ikitokea unahitaji kuiuza nyumba yako makadiriohayataangalia ukubwa wanyumba bali thamani ya nyumba kulingana na mahali ulipo

7. Hakikisha kabla hujaanza ujenzi, angalau unafahamu mambo machache kuhusu gharama na na mna unaweza kupata punguzo badala ya kuwa mgeni kwa kila kitu na kuwategemea mafundiambao baadhi wanaweza kuwa sio waaminifu.

8. Tumia mafundi wazuri na ikifaa wakandarasi waliosajiliwa. Mafundi wazuri na wazoefu ni watu muhimu sana kukusaidia kupunguza gharama zisizo za lazima. 

9. Jitahidi kadiri uwezavyo kupunguza gharama za maandalizi ya site yako zisiwe kubwa sana. Weka mpango sahihi na muda wa kuanza kazi ya ujenzi ili baadhi ya shughuli zichangie gharama. 

10. Jitahidi sana kuepuka mabadiliko mengi wakati ujenzi umeanzanakuendelea kwasababu yatapelekea bajeti yako kutotoshea. 

11. Angaliakimo cha nyumba na upana wake viwe vya kawaida kuweza kuruhusu hewa nzuri ndani kwasababu kadiri nyumba inavyoenda juu zaidi na kutanuka sana ndivyo na paa litakavyohitaji gharama kubwa kulijenga. 

12. Sio lazima kuanzana sakafu za marumaru ama mbao mwanzoni kwa maanahizi zinagharama kubwa. Unaweza kufikiria sakafu ya kawaidanakuweka tile/vigae/marumaru kwenye maeneo muhimu kama jikoni,chooni na bafuni tena kwa urefu mdogo tu. Maboresho zaidi utayafanya baadae

13. Kama unafikiria kuwa na matunzio ya gari ndani, angalainamna ya kufanyaulazima huo kwa magari yote moja au kujengea kijisehemu pembeni (car shed)

Monday, December 19, 2016

Je, unaweza kutofautisha tiles za sakafu na za ukutani!? Tegua kitendawili hapa

Pichani ni ukuta wa uzio wa nyumba (fence) ukiwa umenakshiwa kwa marumaru/tiles.
Yawezekana ukaona ukuta unapendeza lakini usifahamu kama vigae/tiles vilivyotumika havikuwa sahihi.
Kwa jinsi vigae vinavyotengenezwa, hutengenezwa maalumu vikiwa na sifa maalumu kwa matumizi ya eneo maalumu. Kwa mfano, tiles za kujengea sakafuni hutengenezwa kwa kuwa na sifa (properties) zinazowezesha kufaa kwa matumizi ya sakafu kwa watumiaji kukanyaga wakitembea, halikdhalika za ukutani na ndio maana ukienda dukani unaulizia ama tiles zaukutani au za sakafu. Za uutani nazo unaweza lazimika kuulizia ama za bafuni, jikoni au maeneo mengine kwa urembo. Na za sakafuni pia hutegemeana na mahali zinapowekwa.

Kaika picha zetu hizi zinaonesha ukuta umependeza sana,lakinikama utachunguza vizuri utagundua kuwa tiles zilizotumika hapa hazikuwa maalumu kwa ukuta wa nje na baadhi ni maalumu kwa sakafu. 
Lengo la posti hiinikujaribu tu kukumbushana kukumbuka kuwa kuna tofauti ya hizi tiles kutegemeana na matumizi. Siokila wakati tutegemee mafundi pekee watuelekeze. Ni imani yangu kuwa dondoo kama hizi zitakusaidia kupata kilicho bora zaidi.

Baadae nitaweka maelezo kamili ya tilesnaainazakena wapi zitumike zipi!



Wednesday, December 14, 2016

Ujenzi wa sakafu ya mawe ya tanga yaliyokatwa kwa umbo mstatili

Jionee namna mawebapa maarufu kama "Flat Tanga Stone" yanavyoweza kutumika kutengeneza sakafu ya eneola wazi aidha kwa kuegeshea magariau watu kutembelea. Matumizi ya mawe haya yanaweza kuwa kwa 'pattern' tofauti kutegemeana na uhitaji. Unaweza weka ya rangi moja au ukachanganya na ranginyingine. 



Saturday, December 10, 2016

Angalia hapa na Ujifunze Umaridadi mwingine kwa Uzio wa Nyumba yako

Kadiri teknolojiainavyokuwa ndivyo na ubunifu wa mapambo ya nyumba huongezeka. Leo nakusogezeapicha hizi mbili zikionesha urembo mzuri na geti lililopambwa vizuri kuanzia muundo wake na finishin zilizvyofanywa.

Picha ya chini ni rough plaster kwenye ukuta wa tofali kama inavyoonekana. Ukihitaji ufundi wa namna hii ususite kuwasiliana nasi kwa nambari 0757718080 na kuona namna ya kusaidiana kupata kilicho bora! Karibu sana